Chanjo za COVID-19 na wagonjwa wa Kifafa

Chanjo dhidi ya COVID19 sasa zinapatikana. Tunapendekeza kwamba watu walio na kifafa wanapaswa kupokea chanjo ya COVID19 inapopatikana; hii ni pamoja na dozi ya nyongeza. Kwa watu wenye kifafa, hatari ya kuambukizwa COVID-19 na kuzuka kwa madhara zaidi ya kiafya, inapita athari hasi za chanjo ya COVID-19.
Kwa sasa hakuna ushahidi unaoashiria kama, kuwa na ugonjwa wa kifafa kunachangia kuibuka kwa athari hasi kutokana na chanjo ya COVID-19, hasa kuongezeka kwa mshtuko. Lakini, kama ilivyo na chanjo zingine, homa inaweza kuzuka baada ya kupokea chanjo ya COVID-19. Hii inaweza kuongeza matukio ya kuanguka kwa baadhi ya wagonjwa wa kifafa. Lakini, wakitumia madawa ya homa, kama vile Paracetamol /acetaminophen kwa muda wa masaa 48 baada ya chanjo aukipindi chote wanachougua homa, hatari hii inapungua.
Kabla ya kupokea chanjo ya COVID-19, hakikisha umemjulisha anayetoa huduma ya chanjo kuwa wewe ni mgonjwa wa kifafa. Kadhalika mpe taarifa zingine muhimu kuhusu afya yako kama vile;
- mizio haswa mzio dhidi ya kiungo chochote katika chanjo
- mizio yoyote iliyochochewa na chanjo za awali (historia)
- kama una homa yoyote sasa au uliwahi kuugua hivi karibuni
- aina zote za madawa unayotumia (kama kunayo), haswa madawa yanayodhoofisha uwezo wa mwili kujiami dhidi ya magonjwa; au dawa za kuzuia damu kushikamana
- kama u mja mzito (una mimba), unanyonyesha au unanuia kutunga mimba
Kama ilivyo ada na chanjo zingine, usipokee chanjo ya COVID-19 kama una mizio na kiungo chake chochote. Usipokee dosi ya pili kama ulipata mizio kutokana na dosi ya kwanza
Ni muhimu kwa wale ambao tayari wamechanjwa dhithi ya COVID-19, kuendelea kuvaa barakoa, kunawa mikono na kukaa umbali wa mita moja na nusu. Chanzo zinazotumika sasa zinapunguza hatari ya kupata ugonjwa wa COVID-19 kwa takriban asilimia 90 (90%), ikitegemea aina hasa uliyopewa. Walakin, watu waliopokea chanjo ya COVID-19 wanaweza bado kusambaza virusi vya COVID-19 bila kutambua kuwa wanavibeba.
Una weza kupata taarifa zingine muhimu juu ya mada hii katika tovuti hapa:
https://epilepsysociety.org.uk/vaccine
https://www.epilepsy.com/learn/covid-19-and-epilepsy/covid-19-vaccination
https://epilepsysociety.org.uk/news/Covid-vaccine-reassurance
https://livingwellwithepilepsy.com/2020/covid-19/covid-19-vaccine-and-epilepsy.html
Last updated: 17 November 2021
Subscribe to the ILAE Newsletter
To subscribe, please click on the button below.
Please send me information about ILAE activities and other
information of interest to the epilepsy community